Thursday, February 4, 2016

Uchaguzi Mameya Kinondoni na Temeke sasa Kurudiwa

Uchaguzi wa umeya katika Manispaa za wilaya za Temeke na Kiondoni utarudiwa baada ya kugawanywa na kuzaa wilaya za Ubungo na Kigamboni.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene, alisema Rais John Magufuli ameridhia kuanzishwa kwa wilaya hizo pamoja na mkoa mpya wa Songwe.
Aidha, alisema ameridhia kuanzishwa kwa wilaya mpya ya Kibiti (Pwani), Malinyi (Morogoro) na Tanganyika (Katavi).
Alisema mchakato wa kuanzishwa kwa maeneo mapya ya utawala ulihitimishwa kwa kutolewa na tangazo la serikali kwa GN 69 ya Januari 29, mwaka huu, ya kuanzisha kwa mkoa wa Songwe na GN namba 68 ya kuanzishwa kwa wilaya za Songwe, Kibiti, Ubungo, Kigamboni, Malinyi na Tanganyika.
Simbachawene alisema Mkoa wa Songwe umeanzishwa kwa mujibu wa sheria, hivyo hivyo kwa wilaya za Songwe, Kibiti, Ubungo, Kigamboni, Malinyi na Tanganyika.
Kuhusu uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, alisema utarudiwa Februari 8, mwaka huu.
Alisema baada ya kugawanywa kwa wilaya hizo ni dhairi kuwa, baadhi ya madiwani itabidi wakae kwenye halmashauri zao ambazo zinaanzishwa.
Alisema hivi karibuni atateua wakurugenzi wa halmashauri hizo na baadhi ya watendaji muhimu.
Simbachawene alisema amewaagiza wakuu wa mikoa wote ambao katika mikoa yao imeanzishwa wilaya mpya kufanya maandalizi muhimu ili kuwezesha mikoa na wilaya hizo kuanza rasmi.
Katika agizo hilo, ameweka mkazo uwekezwe kwenye upatikanaji wa majengo ya ofisi na huduma muhimu ili kuweka mazingira ya shughuli za kiutawala kuanza kufanyika katika maeneo hayo ya kiutawala.

Mbowe Na Zitto Kabwe Wazika Rasmi Ugomvi Wao Wa Muda Mrefu

Uhasama  uliodumu kwa muda mrefu kati ya Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo) na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe sasa ni wazi unaonekana kumalizika.

Hali hiyo inatokana na viongozi hao kwa nyakati tofauti jana kuweka ujumbe kwenye mitandao yao ya kijamii ya facebook na twitter, ambao unaonyesha kila mmoja akijutia makosa yake na kutaka waungane kwa ajili ya kutetea masilahi ya taifa.

Tangu kuanza kwa mijadala mbalimbali bungeni mjini Dodoma wiki iliyopita, Mbowe na Zitto wameonyesha kukubaliana katika misimamo yao na hivyo kuzua maswali kwamba huenda mbunge huyo wa Kigoma Mjini anataka kujiunga na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Mbowe ambaye pia ni kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, akiwa na Zitto wiki iliyopita waliwaongoza wabunge wengine wa Ukawa kususia kikao cha Bunge kupinga hatua ya Serikali kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya Bunge kupitia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Baadaye viongozi hao pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia, waliitisha mkutano na waandishi wa habari kueleza umma ambavyo Serikali inarudisha taifa katika zama za udikteta kwa kuzuia haki ya wananchi kupata habari.

Katika kikao hicho cha Bunge, Serikali kupitia kwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye, ilitoa taarifa kuwa wanasitisha matangazo hayo ya moja kwa moja ili kubana matumizi ya Serikali yanayofikia zaidi ya Sh bilioni nne kwa mwaka.

Katika ukurasa wake wa facebook na twitter jana, Zitto alinukuu ujumbe wa Mbowe  ambao ulitafsiriwa kwamba ni hatua ya kiongozi huyo wa upinzani kutaka kumaliza tofauti zake za kisiasa na mbunge huyo.

“Kushirikiana na Zitto si jambo la ajabu kama ambavyo umeona tukifanya. Yapo majeraha mengi ambayo tumeyapitia pande zote (Chadema na Zitto) ambayo huwezi kuyatibu kwa siku moja. Yapo ambayo yatapona kulingana na muda. Unaweza kumfanyia mtu kitu kibaya, lakini baadaye ukatambua kuwa umekosea. Chochote katika siasa kinawezekana,” aliandika Mbowe.

Jana kupitia ukurasa wake wa facebook, Zitto ambaye pia ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, alisema nafasi ya chama chake bungeni ni upande wa upinzani hivyo atakuwa pamoja na Ukawa.

“Mbowe siku zote amekuwa kiongozi wangu na siwezi kubeza nafasi yake katika kujenga demokrasia nchini. Tulipishana, tulikoseana, tusameheane.

“Mimi binafsi siwezi kuwa mfungwa wa magomvi yetu ya miaka ya nyuma. Nilishasamehe walionikosea na kuomba radhi niliowakosea.

“Tunaweza kupishana kwenye mkakati wa utekelezaji, hatuwezi kupishana kwenye masilahi ya nchi yetu ya kujenga demokrasia na kukataa udikteta.

“Nafasi ya ACT-Wazalendo bungeni ni upande wa upinzani, na hivyo tutakuwa na wenzetu wa upinzani kwenye kujenga hoja zote za kitaifa.

“Mimi nikiwa mbunge wa ACT-Wazalendo, natekeleza kwa vitendo maelekezo ya chama kwa kushirikiana na wabunge wenzangu wa upinzani bungeni.

“Chama chochote makini huweka tofauti binafsi pembeni kwa masilahi mapana ya taifa. Chama cha ACT-Wazalendo kinaamini katika umoja,”alisema Zitto.

Zitto alifukuzwa Chadema na kujiunga na ACT-Wazalendo Machi 21, 2015 chama ambacho hakina ushirikiano na vyama vinavyounda Ukawa, lakini ameonekana kuwa karibu na umoja huo katika vikao vya Bunge la 11 vinavyoendelea mjini Dodoma.

Mwaka 2013, mwanasiasa huyo machachari pamoja na aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema, Profesa Kitila Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba walifukuzwa kwenye chama hicho, baada ya mfulululizo wa muda mrefu wa mivutano ya uongozi na baadaye wakaanzisha chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT) mwaka 2014.

Chadema ilichukua uamuzi huo baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutupilia mbali pingamizi la Zitto dhidi ya Kamati Kuu kutojadili uanachama wake.
Mpekuzi blog

Magufuli challenges coffee farmers to raise quality, quantity

The Minister for Agriculture, Livestock and Fisheries, Mwigulu Nchemba
 PRESIDENT John Magufuli has challenged coffee farmers in Tanzania and elsewhere on the continent to improve the quality and quantity of their produce if they are to compete in the global market.
 
In a speech delivered on his behalf by the Minister for Agriculture, Livestock and Fisheries, Mwigulu Nchemba during the opening of the 14th African Fine Coffee Conference (AFCA) yesterday in Dar es Salaam, the president said coffee cultivation should be taken as a serious commercial venture.
 
The president emphasised that coffee farming should be a profitable business but quality and quantity must be improved.
 
“We are naturally endowed with suitable climate and excellent soils for coffee production, therefore there is no reason for not increasing coffee production both in quality and quantity,” he said
Further, president Magufuli underscored the need for Tanzania as well as other African countries to diversify their coffee markets by promoting local consumption and look beyond the traditional markets. 
 
“New markets are reported growing fast in the booming economies of East Asia such as China and other countries which represent huge market demand because of the growing middle class in these countries you must tap into these,” the president urged. 
 
The president was keen to warn coffee stakeholders that certification and traceability of coffee exports will soon become a pre-condition to sell the product and they must comply. In the same vein, he urged associations like AFCA to support the initiative so the commodity is certified.
 
“You need to strengthen good trade relationship between producers and consumers for the purpose of sustainability of the coffee industry. Producers have always been complaining of being at a disadvantage when it comes to value sharing and this poses a risk to sustainability of the coffee industry,” he warned.
 
The president paid tribute to AFCA noting that since its inception in 2000, its contribution to the coffee sector in member countries has been significant.
 
“Tanzania is highly appreciative of the continued cooperation and support that AFCA and development partners have offered in improving the coffee sector through manpower training, technology sharing and financial support. Without adequate knowledge, technical and financial support in this area, increase in production and quality would not be possible,” he said.
 
Tim Schilling, Executive Director of World Coffee Research said the coffee sector on the continent has greatly improved over the past decade and attributed the improvement to support from Bill & Melinda Gates Foundation and European Union.
SOURCE: THE GUARDIAN

Employers unhappy with law covering foreign workers

The Minister of State in the Prime Minister's Office (Policy, Parliamentary Affairs, Labour, Employment, Youth and the Disabled), Ms Jenista Mhagama
 Tanzanian employers have voiced their concern over the high fees they have to pay to secure and even renew working permits for their foreign employees.
 
The employers say such fees have increased the cost of doing business in the country, urging the government to review them.
 
They also insist that there are some ‘key’ technical jobs and roles that can be better done by foreigners than locals.
 
“We are faced with a heap of challenges which, honestly speaking, continue to make it very complicated to run a business in Tanzania,” stated Dr Aggrey Mlimuka, executive director of the Association of Tanzania Employers (ATE).
 
Opening a seminar for ATE members here yesterday, Dr Mlimuka said although the association was committed to creating more jobs in the country, the existing local business environment made it difficult to do so.
 
He cited legislation like the Non-Citizens (Employment) Regulations Act of 2015 which, according to him, was extremely unpopular among employers.
“At the risk of being labeled anti-local, we as an association would love to see more relaxed labour and migration laws for foreigners working in the country, vis-à-vis the lack of qualified Tanzanians in specialised fields of work,” he said.
 
Towards the end of last year, the minister responsible for, among other things, labour and employment, Jenista Mhagama, issued a 14-day notice for local companies engaging foreign workers to ensure all of them had valid permanent work permits. 
 
She said the government was acting on reports of foreigners working in the country without valid work permits, or using ‘carry on temporary assignment’ permits.
 
“We would like to inform all employers in the country that under the Non-Citizens (Employment) Regulations Act of 2015, only the Labour Commissioner has the authority to issue work permits and no other person,” Mhagama asserted in a public notice published by the local media.
 
She reminded employers that persevering with foreign workers without valid work permits or holding only ‘carry on temporary assignment’ permits was against the country’s immigration laws.
 
Said Dr Mlimuka: “At the end of the day, it shouldn’t matter where the expertise is coming from, since the issue at hand is a committed workforce in general which contributes towards the development of our country.” 
The ATE boss also expressed concern over the Skills and Development Levy, saying it was too high compared to other countries within the East African Community.
 
According to Dr Mlimuka, ATE has for the past couple of years lobbied for the levy to be further reduced from the current 5 per cent of gross employee salary emoluments. It originally stood at 6 per cent before being pruned to 5 in the 2013/14 financial year.
 
“We strongly believe that reducing the levy further, say from 5 per cent to 2 per cent, will greatly stimulate compliance and encourage formal business, thereby broadening the tax base,” he said, noting that in Kenya the levy stood at only one per cent while it was non-existent in Uganda.
 
Another law he cited as needing amendment was the Employment and Labour Relations Act of 2004, particularly in regard to guidelines on how to treat breastfeeding working mothers.
 
Whereas the law is clear on the duration and frequency of maternity leaves, Dr Mlimuka said it was still vague on the issue of when mothers should be given time off for breastfeeding and how much time they should be allowed.
 
He noted that the issue was considered counter-productive by many employers who, as a result, were often hesitant to hire female employees over males.
 
Representing over 1,300 members from various job sectors in the country, ATE looks out for the interests of employers in matters covering labour relations.
 
 
SOURCE: THE GUARDIAN

Wednesday, February 3, 2016

Mahakama Ya Rufaa Kuamua Ugomvi Wa Nyumba Kati Ya Afande Suleiman Kova Na Godfrey Nzowa


Mahakama ya Rufaa wiki ijayo inaanza kusikiliza kesi za rufani 50 za jinai na madai katika Kanda ya Arusha ikiwamo rufaa ya makamishna wawili wa Jeshi wa Polisi wanaogombea nyumba ya serikali iliyopo Uzunguni Arusha.

Maofisa hao, Godfrey Nzowa ambaye ni Mkuu wa Kikosi cha Kupambana na Dawa za Kulevya katika Jeshi hilo amemshitaki mahakamani aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova akipinga kuuziwa nyumba hiyo. Kamishna Kova hata hivyo amestaafu rasmi mapema mwaka huu.

Kwa mujibu wa orodha ya kesi zitakazosikilizwa na majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa kwa mwezi mmoja mjini hapa, Nzowa anamlalamikia Kova na wenzake kupinga kuuziwa nyumba hiyo aliyokuwa akiishi alipokuwa Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (RCO) wa Mkoa wa Arusha.

Nyumba hiyo aliuziwa Kamishna Kova akiwa ameshahama mkoani Arusha na wakati inauzwa Nzowa alikuwa akiishi katika nyumba hiyo, familia yake akiwa RCO kabla ya kuhamishiwa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuendelea na wadhifa huo, Kova akiwa bosi wake.

Orodha hiyo yenye jumla ya mashauri 50 inaonesha mahakama hiyo itasikiliza rufani ya Wakili maarufu jijini Arusha, Median Mwale ambaye amekata rufaa dhidi ya Jamhuri katika kesi yake ya kudaiwa kutakatisha fedha chafu na kujipatia mabilioni ya fedha kwa njia ya udanganyifu akiwa na wenzake watatu.

Rufani hiyo namba 395 ya mwaka 2013 ya Wakili Mwale dhidi ya Jamhuri imepangwa kusikilizwa na majaji watatu, Mbarouk Salim Mbarouk, Bernard Luanda na Semistocles Kaijage watakaosikiliza pia mashauri mengine kabla ya kutoa uamuzi Machi 5, mwaka huu.

Orodha iliyotolewa na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufaa, E.Y. Mkwizu inaonesha kesi nyingine yenye mvuto ni ile ya wafanyabiashara Philemon Mang’ehe na Gesso Bajuta iliyodumu kwa miaka 20 sasa.

Katika kesi hiyo, Mang’ehe wa Kampuni ya Bukine anamdai fidia ya mamilioni ya fedha Bajuta baada ya kudai kuharibiwa biashara yake ya kusambaza vifaa vya ofisi katika Mahakama ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) mwaka 1996.
Mpekuzi blog

Breaking News...Zitto Kabwe Atangaza Kusameheana na Freeman Mbowe...


Zitto Kabwe Akipeana Mikono na Mbowe
Kupitia ukurasa wake wa Facebook muda mchache uliopita, Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe ameweka picha yake na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe na kuandika hivi; "Mimi binafsi siwezi kuwa mfungwa wa magomvi yetu ya miaka ya nyuma. Nilishasamehe walionikosea…Mbowe siku zote amekuwa Kiongozi wangu na siwezi kubeza nafasi yake katika kujenga demokrasia nchini. Tulipishana. Tulikoseana. Tusameheane"

Tulia utafakari, halafu tupe maoni yako

Tigo Yawapa Wateja wake Huduma ya WhatsApp bure


Meneja Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Tigo, Diego Gutierrez akizungumza na waandishi wa habari na wageni waalikwa  mbalimbali wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo uliofanyika jana  Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam 
 Wafanyakazi wa Tigo na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakifurahia jambo  wa uzinduzi wa huduma ya whatsapp bure kwa wateja wa tigo iliyofanyika jana katika hotel ya Hyatt Regency Jijini Dar es salaam
 Hapa kila mgeni mualikwa akiwa busy na simu yake kwenye uzinduzi huo.
 Ni kama wanasema 'tumependeza sana ngoja tujipige picha'  wakati wa uzinduzi wa huduma ya whatsapp bure kwa wateja wa tigo iliyofanyika jana katika hotel ya Hyatt Regency Jijini Dar es salaam

.
Wageni waaalikwa wakiwa katika maski za  " Emojis " wakifurahia jambo kwenye uzinduzi   huduma ya whatsapp bure kwa wateja wa tigo iliyofanyika jana katika hotel ya Hyatt Regency Jijini Dar es salaam
 Hapa ni furaha tupu kwa wanahabari.
 Washereheshaji katika uzinduzi huo,Mc  Taji Liundi na Mc Abby wakitoa maelezo jinsi gani wateja wa Tigo watakavyofurahia huduma ya whatsapp bure 
 Burudani ikiendelea kutoka kwa wasanii wa kikundi maalum cha maonesho ya jukwaa  wakati wa uzinduzi wa huduma ya whatsapp bure kwa wateja wa tigo iliyofanyika jana katika hotel ya Hyatt Regency Jijini  Dar es salaam.
 Meneja Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Tigo, Diego Gutierrez  (katikati), akiwa na viongozi wenzake kutoka tigo katika maski za "Emojis " wakati wa uzinduzi wa huduma ya whatsapp bure kwa wateja wa tigo iliyofanyika jana katika hotel ya Hyatt Regency Jijini Dar es salaam
  Meneja Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Tigo, Diego Gutierrez  (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na washereheshaji MC Taji Liundi na MC Abby  wakati wa uzinduzi wa huduma ya whatsapp bure kwa wateja wa tigo iliyofanyika jana katika hotel ya Hyatt Regency Jijini Dar es salaam

 Ofisa Mkuu wa Biashara wa Tigo, Shavkat Berdiev (kushoto )  Meneja wa gharama  wa Tigo Jakhangic Tulaganov  na Meneja masoko Olivier prentout wakifurahia jambo wakati wa uzinduzi wa huduma ya whatsapp bure kwa wateja wa tigo iliyofanyika jana katika hotel ya Hyatt Regency 
Bloggers wakiwa katika picha ya pamoja na msanii Lucas  Muhuvile 'Joti'  wakati wa uzinduzi wa huduma ya whatsapp bure kwa wateja wa tigo iliyofanyika jana katika hotel ya Hyatt Regency



Dar es Salaam, Februari 2, 2016- Kampuni ya Tigo Tanzania ambayo inaongoza kwa mtindo wa maisha ya kidijitali imetangaza huduma ya bure ya WhatsApp kwa watumiaji wa huduma hiyo  ikiwa ni mara ya kwanza kwa kampuni ya simu  kutoa ofa ya bure  ya mtandao huo wa jamii  nchini.

 Akitangaza upatikanaji bure wa huduma hiyo kwa vyombo vya habarijijini Dar es Salaam, Meneja Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez amesema kuwa wateja wote wa Tigo  wanaotumia  vifurushi vya intaneti  vya kampuni hiyo kwa wiki na mwezi  watapata huduma ya WhatsApp bure. Tigo ina wateja zaidi ya milioni 10.

Huduma ya WhatsApp ambayo ni maarufu kwenye kutuma ujumbe  kwa njia ya simu, ina watumiaji zaidi ya milioni nane nchini Tanzania  na  duniani  inatumiwa na watu wapatao milioni 900. WhatsApp inawezesha watumiaji  kubadilishana habari, ujumbe, video na miito ya sauti.

“Kuanzia sasa na kuendelea wateja wote wa Tigo wanaonunua vifurushi vyetu vya wiki au mwezi  watakuwa na fursa ya kufurahia  WhatsApp BURE. Hili linawezekana kama mteja ana smartphone. Huduma ya bure ya WhatsApp kwa wateja wetu inaonesha  jinsi tulivyojikita katika kuboresha mabadiliko kwenye  maisha ya kidijitali  na hivyo kuongoza kwenye kutoa teknolojia ya hali ya juu pamoja na ubunifu”, alisema Gutierrez.

Kwa Mujibu wa Gutierrez, ili kufurahia huduma hii, jambo analohitaji mteja wa Tigo ni kuwa na  kifurushi cha intaneti  cha wiki au mwezi  ambacho anaweza kukipata kupitia *148*00# àTigo-Tigo Xtreme/MiniKabangà Wiki au Mwezi + WHATSAPP YA BURE. Huduma hii inapatikana kwa wanaomiliki simu  za aina ya Blackberry, Android na Nokia Symbian60.


WhatsApp ni huduma dada na huduma huduma Facebook ambayo iliingia makubaliano na Tigo mwaka 2014 na kuwapa fursa wateja wa Tigo huduma ya Facebook bure na kwa lugha ya Kiswahili kupitia simu zao.
Powered by Blogger.