Mwenyekiti wa Kikosi kazi kinachoshughulikia udhibiti utoroshwaji wa madini ya Tanzanite nje ya nchi, Muliro Muliro (aliyesimama) ambaye pia ni Afisa Upelelezi wa Makosa ya Jinai mkoani Arusha, akitoa taarifa ya Kikosi Kazi hicho kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Manyara, Arusha na Kilimanjaro, Amos Makala (wa kwanza kulia) wakati wa kikao cha Kamati hizo kilichofanyika jijini Arusha.Wengine katika picha ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (wa pili kulia) na wa Tatu kulia ni Kaimu Kamishna wa Madini nchini, Mhandisi Ally Samaje.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati za Ulinzi na Usalama za mikoa ya Kilimanjaro, Manyara na Arusha wakiwa katika kikao cha Kamati hizo kilichofanyika katika kituo cha Jimolojia mkoani Arusha. Kamati hizo zinashirikiana na Wizara ya Nishati na Madini katika kudhibiti utoroshwaji wa madini ya Tanzanite nje ya nchi na ukwepaji kodi unaofanywa na kampuni zinazoshughulika na biashara ya madini nchini.
0 comments:
Post a Comment