Sunday, March 26, 2017

Fahamu Mambo Matano ya Kushangaza Kuhusu Tangawizi

Image may contain: 3 people, people sitting and closeup




TANGAWIZI ni kati ya viungo mahili vinavyochochea ladha nzuri katika vyakula vya aina mbalimbali na hivyo kuwavutia walaji kula chakula husika.

Tangawizi pia inapowekwa kwenye vyakula vigumu kama nyama huifanya ilainike na hivyo kuweza kuiva kwa haraka zaidi. Hivyo kwa point hiyo tu kwanza utagundua kiungo hiki pia kinaweza kurahisisha umeng'enyaji wa chakula tumboni pia

Wakati tangawizi ikiwa inafahamika zaidi kama kiungo, kwa upande mwingine kiungo hicho huweza kupunguza athari za matatizo mbalimbali ya kiafya pia kama ifuatavyo kwenye orodha hii hapa chini:-

1. Hupunguza maumivu kwa wanawake wakati wa kipindi cha hedhi (Period)

2. Huppunguza maumivu ya mifupa pamoja na misuli kwa ujumla.

3.Inaelezwa kusaidia kuimarisha uwezo wa utunzaji wa kumbukumbu kwa binadamu.

4. Husaidia kutuliza maumivu ya tumbo pia

5. Husifika kwa kuimarisha kinga za mwili na kuufanya mwili kupambana vizuri dhidi ya magonjwa

Tuesday, March 21, 2017

Eheee..Askofu Gwajima Kutimba Clouds Kesho,Atoa Ujumbe Huu Mzito Kwenye Instagram...!!



Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Bishop Josephat Gwajima amesema kuwa Jumatano hii atatembelea Clouds Media Group kwajili ya kuwapa pole kwa yaliyotokea hivi karibuni.

Ijumaa iliyopita kituo hicho kilivamiwa na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akiwa na askari wenye mitutu kitendo kilichopingwa na wadau mbalimbali wa habari.

“Kesho Tarehe 22/03/2017 saa nne kamili asubuhi, nitatembelea Ofisi za Clouds Media ili kuwapa pole kwa yaliyotokea.” aliandika mchungaji huyo kupitia ukurasa wake wa Instagram.


Yanga Fungu la Kukosa ,Yapangwa na Waarabu Kombe la Caf...!!!




Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) limetoa ratiba ya mechi za kombe la shirikisho. Katika ratiba hiyo klabu ya soka ya Yanga imepangiwa kucheza na MC Alger kutoka Algeria.

Yanga imeingia katika hatua hiyo baada ya kutolewa katika kombe la klabu bingwa barani Afrika na Zanaco kutoka Zambia Jumamosi hii.

Timu 32 zimeingia katika hatua hiyo ambapo mechi zake zinatarajiwa kuchezwa kati ya April 7-9 na marudiano April 14-16. Vilabu 16 ndio vinahitajika ambavyo vitaingia katika hatua ya makundi ya kombe hilo

Rais wa Zambia Apigiwa Magoti na Waziri Wake...!!!


Rais wa Zambia Edgar Lungu akinyenyekewa na waziri wake wa Mifugo na uvuvi,

Monday, March 20, 2017

Breaking Newss..Wabunge wa CCM Dalaly Kafumu na Vicky Kamata Wajiuzulu,Waandika Barua Zenye Ujumbe Mzito Kuhusu Serikali ya Magufuli...!!!



Mwenyekiti Kamati ya Kudumu ya Bunge, Viwanda na Biashara, Dkt. Dalaly Peter Kafumu, makamu mwenyekiti wa Kamati hiyo, Vicky Kamata wamejiuzulu nyadhifa zao hizo leo Machi 20, 2017.

Wabunge hao wamesema wamefanya uamuzi huo ili waweze kupata muda wa kutosha kuwatumikia wananchi majimboni mwao.

Aidha viongozi hao wameeleza sababu za kuchukua hatua hiyo kuwa ni serikali kuingilia majukumu yao katika utendaji kazi na hivyo wakaeleza kuwa hawaoni sababu za kuendelea na majukumu hayo.
Kafumu ni Mbunge wa Jimbo la Igunga (CCM) ambapo Vicky Kamata ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM) akiwakilisha wanawake wa Mkoa wa Geita.

Wamekabidhi barua za kujiuzulu kwenye ofisi ya spika wa bunge jana.

Kudadadeki..Makonda Azidi Kupigwa Kila Kona..Machangudoa Waungana Kuanzisha Mtandao Huu Hatari Ili Kumkabili...!!!!





BAADA ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuelezea mafanikio aliyoyapata, changamoto alizokutana nazo na mipango inayofuata ya mwaka wake wa pili aliouanza, wanawake wanaofanya biashara ya ‘uchuuzi wa mwili’ (machangudoa), wameibuka na mbinu mpya ya kumdhibiti kiongozi huyo ili asiwabughudhi.

Uchunguzi uliofanywa na Risasi Jumamosi umebaini kwamba, baada ya kuchoshwa na kukimbizwa na kukamatwa na polisi chini ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, CP Simon Sirro wanapojiuza barabarani kwa amri ya Makonda, sasa wameanzisha mtandao wa kujiuza ambao unaelezwa ni hatari zaidi.

“Unaambiwa sasa hivi mambo ni kidijitali na ni vigumu kuwakamata kwani huwezi kumtambua mwanamke anayejiuza kirahisi kwa sababu mchongo mzima unachongwa mtandaoni kupitia Mitandao ya Kijamii ya Instagram na WhatsApp na siyo kusimama barabarani kama zamani.

“Wenyewe wanasema wamempiga tobo Makonda kwa kubuni njia mpya ya kuwaingizia kipato, tena bila kujidhalilisha kama zamani,” alitonya mtoa taarifa wetu hivyo kutoa ‘asainmenti’ kwa Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers.

OFM KAZINI Ikiwa kazini, OFM ilitonywa kuwa kwa sasa kuna mbinu mpya ambayo machangu wanatumia kwa sasa hasa wa maeneo ya Sinza ambao wametoweka katika vijiwe vyao kisha kujituliza magetoni kwao kusubiria oda kutoka kwa wanaume hivyo kuwataka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na polisi kuingilia kati kukomesha ishu hiyo.

“Hivi mnajua kuwa machangu siku hizi hawaonekani kwenye maeneo yao ya usiku? Unajua kuna kipindi walizidi mno lakini kufuatia udhibiti wa polisi chini ya Makonda wa kuwapitia na kufunga maeneo, sasa wameunda magrupu tofautitofauti mitandaoni na kuwavuta wateja wao kirahisi. WANAFANYAJE? ”

Ishu nzima ipo hivi, wanajitangaza kwa kuanika picha zao za utupu na nusu utupu pamoja na vipande vya video kwenye Instagram kisha wanakuwekea namba zao za simu na kukutangazia, ukitaka kujiunga kuwaona live unatuma kiasi cha kati ya shilingi 5,000 hadi 10,000 na ukiingia humo unawakuta kibao hivyo TCRA na polisi kazi wanayo.

“Wapo wanaotoa huduma ya kukuunganisha tena kwa utakayemtaka kwa gharama ya shilingi 10,000 kisha ushindwe mwenyewe tu kwani wapo tu magetoni wanasubiri uingie kwenye kumi na nane zao,” alisema Abdi, mkazi wa Afrika Sana, Dar.

OFM YACHIMBA Baada ya kujua mbinu hiyo, OFM ilijipanga na kumtuma mmojawao ambapo aliingia katika Mtandao wa Instagram na kukutana na makundi mengi ambayo yamewekwa majina ya kukuonesha kuwa huduma hiyo ipo kisha akawatumia kiasi hicho cha fedha na punde akaunganishwa na kushuhudia video na picha za utupu.

MMOJA AINGIA MTEGONI Baada ya kuunganishwa kama yalivyo masharti yao, aliomba apatiwe mmojawao ambapo aliambiwa atoe tena kiasi kingine cha shilingi 10,000 na baada ya kufanya malipo hayo aliunganishwa na mrembo aliyetambulika kwa jina moja la Irene tayari kwa kwenda kujinoma naye.

OFM aliahidiana na Irene kukutana sehemu kwa ajili ya huduma hiyo na kukubali kufika lakini baada ya kuketi katika maongezi, OFM akiwa katika harakati za kuchomoa simu apige picha kadhaa, Irene alishtuka na kuwa mkali kama pilipili ambapo alitaka kumkusanyia watu hivyo OFM kupata wakati mgumu kabla ya mrembo huyo kutimua kwa kumnyeshea mvua ya matusi.

OFM ARUDI TENA KUNDINI Licha ya Irene kushtuka kama anataka kupigwa picha, OFM ilirudi tena katika kundi hilo kwa lengo la kumpata mwingine kwa kuwa alikuwa bado mmoja wa memba hivyo ikawa rahisi kuchukua na namba ya mwingine lakini kila alipokuwa akipigiwa alipokea na kudanganya maeneo alipo.

WASIKIE TCRA Baada ya kujiridhisha kuwepo kwa mbinu hiyo mbadala OFM iliwasiliana na Meneja Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy ambaye alisema kuwa, ishu hapo ni kuwe na mtu wa kwenda kulala kwenye Kitengo cha Uhalifu wa Kimtandao cha Polisi (Cyber Crime Unity) ambao hao ndiyo wenye idhini ya kumkamata mtu.

KITENGO CHA CYBER Kuhusu ishu hiyo, kamanda wa kitengo hicho, Mwangasa Joshua aliliambia gazeti hili kuwa baada ya kupokea malalamiko juu ya biashara hiyo, jopo lake la uchunguzi litakaa na kuyabaini ‘magrupu’ hayo ili kuyachukulia hatua kwani Sheria ya Makosa ya Mtandao ipo na inafanya kazi.

TUJIKUMBUSHE Juni mwaka jana, Makonda alitangaza vita na makakapoa (mashoga) na madadapoa (machangu) walioko jijini Dar kuwa ataendesha msako mkali wa kuwaondoa, jambo lililofanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Credit - Global Publishers

Jenerali Ulimwengu Ashauri Makonda Ashitakiwe kwa Kuvamia Kituo cha Clouds...!!!



Akihijowa na DW mchana huu Jenerali Ulimwengu ameshauri Makonda ashitakiwe...

Amesema ni tukio linaloweza kufanywa na viongozi ambao wanajiona hawana mipaka katika utawala wao. 

Amesema mkuu wa mkoa amelewa madaraka na kwa kufanya tukio hilo ameonyesha kwamba hana kitu chochote kinachoweza kumzuia. Amewaomba wananchi kupata sauti zao katika kutetea haki zao.

Amesema suala la Makonda kuwajibishwa linategemea na mtu aliyemchagua ambaye ndiye kiongozi wa nchi kwa hiyo Raisi akiona kwamba kuna haja ya Makonda kuwajibishwa basi amuwajibishe ili iwe fundisho na kwa viongozi wengine.

Nape Nnauye : Hili Likinishinda Hakika Nitajiuzulu



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye amesema endapo atashindwa kusimamia uhuru wa habari na vyombo vya habari nchini atakuwa hafai kubaki kwenye nafasi hiyo kwa kuwa atakuwa ameshindwa majukumu yake katika nchi huru

Nape ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumzia na kulaani kitendo kinachodaiwa kufanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, cha kuvamia chombo cha habari cha Clouds, akiwa na askari wenye silaha na kukifananisha kitendo hicho na kuinajisi taaluma ya habari.

Waziri huyo amesema amezoea kuona matukio kama hayo yanatokea kwenye nchi ambazo zimepinduliwa kwa bunduki lakini kwa nchi yetu si jambo jema kwenda kwenye vyombo vya habari na mabunduki mkononi.

"Tumezoea kuona matukio haya yanatokea kwenye nchi ambazo zimepinduliwa kwenda kwenye vyombo vya habari na mabunduki si sawa, kwa jambo hili tunataka kutenda haki tumsikilize Mkuu wa Mkoa ili tujue kwanini amefanya jambo hili". Alisema Nape

Kufuatia tukio hilo Waziri Nape ameunda tume yenye w

Alichosema Rais Magufuli Kuhusu Paul Makonda Leo



Tofauti na kile ambacho watanzania wengi leo walikuwa wakitarajia kuona Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli akichukua uamuzi mgumu dhidi ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, mkuu huyo wa nchi amemuelezea Makonda kuchapa kazi.

Makonda anakabiliwa na kashfa lukuki ikiwemo ile ya kudaiwa kughushi vyeti na kwamba jina lake halisi ni Daudi Bashite, kutumia vibaya madaraka yake ikiwemo tukio la juzi la kuvamia studio za Clouds Media Group akiwa na wanajeshi wenye silaha akilamizimisha kurushwa kwa kipindi na zingine. Tukio hilo limelaaniwa vikali.

Akizungumza Jumatatu hii kwenye uwekaji jiwe la msingi katika mradi wa barabara za juu (Flyovers) Ubungo, Dar, Rais Magufuli amesema, “Mimi ndio najua mwenyewe nani anatakiwa kuwa wapi akae wapi, ni mimi ninayepanga. Ninajua wamenielewa. Kwahiyo Makonda wewe chapakazi, nasema chapa kazi.”

“Suala la kuandikwa kwenye mitandao sio tija kwangu, hata mimi ninaandikwa kwenye mitandao kwahiyo nijiuzulu urais? Chapa kazi, hapa kazi tu.”

Rais amesema Watanzania wanapoteza muda mwingi kwa mambo yasiyo ya msingi.

“Tumepoteza direction tumeanza kujadili personalities,” aliongeza.

Saturday, March 18, 2017

Yanga Mdebwedo Yatolewa Ligi ya Mabigwa..ila Kushiriki Mashindano Haya




YANGA SC imeangukia Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kutolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa baada ya sare ya 0-0 na wenyeji, Zanaco jioni ya leo Uwanja wa Taifa wa Mashujaa, Lusaka nchini Zambia.

Matokeo hayo yanamaanisha Yanga inatolewa kwa mabao ya ugenini, baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza wiki iliyopita Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Yanga wataumia zaidi kwa kutolewa na Zanaco, kwani bao la kusawazisha la Wazambia hao Dar es Salaam lililopatikana dakika ya 78  kupitia kwa mshambuliaji wake Mghana, Attram Kwame lilikuwa la kuotea.

Na pamoja na hayo, wachezaji wa Yanga walikuwa wamezubaa kusubiri wapinzani wao watoe nje mpira kiungwana (Fair Play) baada ya mchezaji mwenzao, Obrey Chirwa kuangushwa.

Siku hiyo, Yanbga ilitangulia kwa bao la winga Simon Happygod Msuva dakika ya 39 baada ya kuwachambua mabeki wa Zanaco kufuatia pasi nzuri ya kiungo Mzambia, Justin Zulu.

Na ushindi huu unaifanya Zanaco iendeleze rekodi ya kuitupa nje Yanga kwenye michuano ya Afrika, baada ya mwaka 2006 pia kuwatoa katika hatua kama hii ya Ligi ya Mabingwa kwa jumla ya mabao 3-2, wakishinda 2-0 Lusaka baada ya kufungwa 2-1 Dar es Salaam.

Yanga sasa itamenyana na timu iliyofuzu hatua ya 32 Bora ya Kombe la Shirikisho kuwania tikeit ya kucheza hatua ya makundi ya michuano hiyo, wakati Zanaci inakwenda moja kwa moja hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa.
Powered by Blogger.